Tanzania Anthem

Sunday, 15 June 2014

SOMA TAARIFA YA HABARI YA DODOMA FM HAPA


DODOMA
Wakulima wa manispaa ya Dodoma  wameiomba serikali kuboresha mfumo wa uendeshaji  wa zoezi la sensa ya watu na makazi
Wakizungumza na Dodoma fm wakulima wa mkoa wa Dodoma wamesema hawanufaiki chochote tangu kuanzishwa kwa mchakato huo wa sense ya watu na makazi.
Nae bw.  Mafita maulid ameiomba serikali kuboresha huduma mbalimbali za jamii iliwaweze kujua umuhimu wa sense.

Akizungumzia swala hilo  mchambuzi wa masuala ya sensa  Bw Kenedy Nteminyanda  amesema   ni vema sense ya watu na makazi ingesaidia katika kumaliza swala na migogoro ya wakulima na wafugaji.
Wakazi wa manispaa ya Dodoma wametakiwa kujitokeza kwa wingi siku ya kuadhimisha siku ya damu duniani itakayo fanyika tarehe 14 Juni mwaka huu.
Wakizungumza na kituo hiki  bi.Frora kamwela ambaye ni muuguzi na mshauri nasaha wa kitengo cha damu salama amesema  maadhimisho ya siku ya damu Duniani kwa mkoa wa Dodoma yatafanyika katika kituo chao kidogo cha Benki ya Damu.
Aidha Bi. Frola amesema a anawaomba watu  wawe na umoja  katika suala la kuchangia damu kwani  suala la kuchangia damu salama ni jukumu letu sote.
Pia amesema kuwa  endapo utajitokeza  katika suala zima la kujitolea damu salama utapata kadi na itakusaidia popote uendako nchini kama utakuwa na tatizo la kutaka damu utapewa bila gharama yeyote.
Sanjari na hayo  Bi.Frola kamwela amesema kila mmoja anaruhusiwa kutoa damu isipo kuwa mtu mwenye  tatizo la sukari,presha ya kupanda au ya kushuka,pamoja na magonjwa mengine.
Serikali kupitia wizara ya ardhi nyumba maendeleo na makazi imekiri kuwepo na matatizo ya ardhi isiyopimwa nchini.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Ardhi nyumba maendeleo na makazi  Prof. Anna Tibaijuka alipokuwa akijibu swali la mbunge wa viti maalumu Bi Muhonga Luhanywa lililohoji kwa nini serikali isiwe na mpango wa kupima ardhi ili kuondoa ujengaji holela mijini na vijijini
Aidha Prof. Tibaijuka ametanabaisha kuwa kama sheria namba nane ya mwaka 2007 ya mipango miji ingefuatwa kusingekuwa na ujenzi holela nchini.
Pamoja na hayo Prof. Tibaijuka amesema kwa kupitia mpango wa serikali wa matokeo makubwa sasa ifikapo mwaka 2017 kila kipande cha ardhi kitakuwa kimepimwa.
KITAIFA
Makamu mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Philip Mangula amesema kituo hicho kimekumbwa na mpasuko baada ya vyama vya upinzani kususiakikao kilichoitishwa Jumapili iliyopita.
Kitendo cha vyama hivyo kutoonekana kumetafsiriwa kama mwendelezo wa kile kilichotokea katika Bunge Maalumu la Katiba Aprili 16, baada ya wapinzani kususia vikao kutokana na kutokuridhishwa na mwenendo wa chombo hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za makao makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma Bw. Philip  Mangula ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa CCM, alisema kikao hicho kililenga kujadili mwenendo wa vyama na athari zake kisiasa.
KIMATAIFA                                                                                              
Wapiganaji wa Kiislamu wamedaiwa kuendelea  kuteka maeneo zaidi nchini Iraq, katika hatua ambayo Marekani imetaja kuwa  ni tishio kwa eneo zima.
Polisi  wa Iraq wamesema kwamba muungano wa makundi  hayo - Islamic State of Iraq na Levant - ambao wanajiita kwa pamoja ISIS wameteka mikoa ya Kirkuk na Salehddin.
Inadaiwa kuwa wapiganaji hao tayari wameteka mji mkuu wa pili kwa ukubwa nchini Iraq wa Mosul, Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo.
Wanajeshi na polisi  wanadaiwa kuwa wametoroka baada ya makabiliano makali na wapiganaji hao wa kundi la Islamic State kutoka Iraq na Syria, wanaojulikana kama ISIS, likiwa ni kundi lililochipuka kutoka Al Qaida.
Wapiganaji wa ISIS wamekuwa wakisimamia shughuli za Mkoa wa Mosul kwa njia isiyo rasmi kwa miezi kadhaa sasa, ambapo wametoza kodi kwa bidhaa zote zinazoingia na kuondoka eneo hilo na wakati huohuo kupokea pesa za kutoa ulinzi kwa maafisa wa Serikali katika Mkoa huo.
Majibizano ya risasi yametokea katika meli iliyobeba wahamiaji haramu 300 katika ghuba ya Bengal na kusababisha idadi isiyojulikana ya watu kujeruhiwa.
 Meli hiyo imekwama katika kisiwa cha Saint Martin, mji wa Teknaf ulioko wilaya ya Cox Bazaar nchini Bangladesh.
Luteni Kazi Harunur Rashi wa kikosi cha ulinzi wa pwani ya Teknaf amesema, walipewa taarifa kuwa meli hiyo imekwama baada ya kupata ajali ikiwa na abiria 300 ambao walikuwa wanaelekea nchini Malaysia kutafuta maisha bora.
Taarifa zaidi kuhusu uraia wa abiria hao na chanzo cha majibizano ya risasi hazijapatikana.
Rais wa Sudan Kusini Salva Kirr na kiongozi wa waasi Riek wamekubaliana kufanya mazungumzo ya kubuni serikali ya mpito ya umoja wa kitaifa.
Mwenyekiti wa jumuiya ya ushirikiano wa kiserikali wa nchi za mashariki na pembe ya Afrika IGAD, waziri mkuu wa Ethiopia Hailemarriam Desalegne, amesema kuwa uamuzi huo umefikiwa kwa lengo la kukomesha vita huko Sudan Kusini.
Baada ya mkutano wa zaidi ya saa nne katika ikulu ya waziri mkuu wa Ethiopia, mwenyeji wa mkutano huo Hailemarriam Desalegne ametangaza kuwa Kirr na mwenzake Machar wako radhi kushirikiana.
Ni kwa sababu hiyo vikao vitaanza Addis Ababa baina ya washirika wa Salva Kirr, Riek Machar na wale kutoka katika mashirika ya kijamii kujadili jinsi ya kuirejesha Sudan Kusini katika njia ya  amani.
Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa viongozi hao wawili kukutana tangu watie mkataba wa kusitisha vita nchini Sudan Kusini.
Shirika la IGAD ambalo limekuwa likiongoza juhudi za upatishi katika mzozo huo uliodumu kwa miezi saba, limeruhusu umoja wa mataifa kutuma vikosi vya usalama nchini Sudan kusini, kulinda amani kama inavyohitajika kutoa ulinzi kwa waangalizi nchini humo..

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive