Imeelezwa kuwa chombo cha mahakama
kuchelewa kuwajibika ipasavyo katika kutoa maamuzi ya ma
shauri katika mahakama Mikoa ya Rukwa na Katavi kumekuwa chanzo cha wananchi kujichukulia sheria mkononi dhidi ya waharifu.
shauri katika mahakama Mikoa ya Rukwa na Katavi kumekuwa chanzo cha wananchi kujichukulia sheria mkononi dhidi ya waharifu.
Hayo yamebainishwa leo na Jaji
Mfawidhi Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Sumbawanga Kakusulo Sambo katika
kikao cha Balaza la wafanyakazi wa mahakama kanda ya Sumbawanga ambacho
kimefanyika Mjini Mpanda.
Aidha,Jaji Sambo amesema Mahakama kuu kanda ya Sumbawanga
imeweka mikakati ya kuamua mashauri yote yaliyopo mahakama za Mikoa ya Rukwa na
Katavi kuanzia mashauri yenye miezi 18-miaka 10 ambapo yanatarajiwa kuamuliwa kuanzia
mwezi machi mpaka mwezi Desemba mwaka huu.
Jaji Sambo ameongeza kuwa baada ya maazimio
yaliyoafikiwa katika kikao cha majaji kilichofanyika Mkoani Mwanza mwezi Novemba
mwaka jana ya kutochelewesha mashauri ya kesi,pia mwezi ujao majaji mafawidhi
wa mahakama nchini wanatarajia kukutana
kwa ajili ya kutoa taarifa mbalimbali za utekelezaji wa maamuzi ya mashauri
yaliyopo mahakamani.
Wakati huohuo taarifa ya Naibu
Msajili Mahakama kuu kanda ya Sumbawanga inaonesha Mahakama ya Wilaya ya Mpanda
inaongoza kwa mashauri 438,ukilinganisha na Mahakama ya Wilaya ya Nkasi yenye
mashauri 373 huku Mahakama ya Wilaya ya Sumbawanga ikiwa na mashauri 78 huo
ukiwa ni wastani wa kesi kwa mwaka.
0 comments:
Post a Comment