Tanzania Anthem

Thursday, 26 March 2015

10,961 Mkoani Katavi wanaishi na Virusi vya UKIMWI

Na Agnes mnubi-katavi
Jumla ya  watu 10,961 Mkoani Katavi wanaishi na Virusi vya UKIMWI ikiwa ni takwimu za Mkoa kwa mwaka 2014.

Takwimu hizo Zimetolewa na Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi  DKT GABRIEL CHENGULA wakati akihojiwa na Sauti ya Katavi ofisini kwake  ili Kujua takwimu za Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi Mkoani hapa.

Dkt. Chengula amesema kuwa Idadi ya watu walioambukizwa Virusi vya Ukimwi Mkoani KATAVI huongezeka Kila mwaka ambapo kwa mwaka 2013 idadi ya watu waliokuwa wameambukizwa  walikuwa 5,389.

Pia Dkt Chengula amesema sababu Kubwa ya Kuongezeka kwa Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi Kunatokana na watu Kutojitokeza Kupima ili kujua afya Zao.

Aidha Chengula ameongeza kusema kuwa uhaba wa watumishi wenye ujuzi , wagonjwa kutotumia dawa kwa usahihi kadri ya maelekezo waliyopewa, kukatiza matumizi ya dawa pamoja na wagonjwa kuikataa hali yao ya ugonjwa ni miongoni mwa changamoto wanazokabiliana nazo wakati wa kutoa huduma kwa watu  wanaoishi na virusi vya ukimwi.
Kiwango cha Maambukizi ya Ukimwi Katika Mkoa wa KATAVI Ni asilimia 5.9 wakati  wastani wa Taifa Ukiwa ni asilimia 5.1


Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive