Tanzania Anthem

Saturday, 6 December 2014

KUJUA SHERIA ZA KANI NI MHIMU!! SOMA ZAIDI

Waajiri na waajiriwa wametakiwa kutambua haki zao katika maeneo yao ya kazi ili kuepukana na matatizo yasiyo ya msingi yanayojitokezea baina ya muajiri na muajiriwa


Akizungumza na kituo hiki mwezeshaji  masuala ya ujasilia mali yanayofadhiliwa na shirika la kazi duniani ILO Bwana Beny Mwambela amesema kwa sasa waajiri pamoja na waajiriwa wanashindwa kutambua haki zao kutokana na kutozijua sheria za kazi na ndio maana wameona kuna haja ya kumsaidia mjasiria mali mdogo.


Aidha Bwana Mwambela kumekuwa na uoga kwa waajiri pamoja na waajiriwa  juu ya haki zao za msingi kutokana na kutozijua  sheria za kazi zinasema hivyo shirika la kaz duniani,pamoja na shirikisho la waajili nchini likaona umhimu wa kumpatia semina hiyo mjasiria mali.


Kwa upande wao wajasilia mali waliohudhulia mafunzo hayo wamewapongeza waandaji wa semina hiyo na kusema kuwa kwa sasa wanaamini kuwa watapata haki zao na kuwa sheria nyingi walikuwa hawazijui kabla ya mafunzo hayo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive