Tanzania Anthem

Thursday, 25 September 2014

POLISI DODOMA YA OKOTA VIPEPERUSHI VYA UVUNJIFU WA AMANI.


Na Stanley Msigwa                                                           Chanzo jeshi la polisi

Jeshi la polisi mkoa wa Dodoma limesema  leo alfajiri vimeokotwa vipeperushi  maeneo mbalimbali  mjini hapa vyenye  ujumbe unao chochea uvunjifu wa amani.


Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma kamishna msaidizi mwandamizi wa jeshi la polis David Misime amesema wanaendelea kupata taarifa za watu wanao daiwa kuandaa vipeperushi hivyo  na wanalifanyia kazi ili waweze kuwakamata na kufikishwa mahakamani kwa kosa la kutoa vitisho na uvunjifu wa amani.

Aidha kamanda Misime ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Dodoma na wageni waliopo mkoani hapa  watii sheria bila shuruti  kwa kuhakikisha kila mmoja anajiepusha na uhamasishaji wa uvunjifu wa amani kupitia mikusanyiko isiyo halali na maandamano ambayo yamekwisha pigwa marufuku.

Sanjari na hayo amesema jeshi la polisi limejiimarisha ipasavyo kukabiliana na yeyote Yule atakaye kiuka sheria na maelekezo yaliyo tolewa.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive