Tanzania Anthem

Thursday, 24 July 2014

WANANCHI DODOMA WAILILIA DUWASA


Wakazi wa Manispaa ya  Dodoma wameulalamikia uongozi wa mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira DUWASA kwa kuwakatia maji ili hali wakijua wana hali ngumu   ya kiuchumi.
                       .
Wakizungumza na kituo hiki wakazi hao wamesema wamekuwa wakipata changamoto kubwa katika ulipaji wa bili ya maji kutokana na hali ngumu ya kiuchumi hali inayowapelekea baadhi yao kushindwa kabisa kutoa mchango huku wengine wakitoa nusu ya fedha zinazohitajika.
Pia wakazi hao wameiomba Mamlaka hiyo kuwavumilia pindi wanapochelewa kulipa bili kwani wanatambua umuhimu wa maji lakini hali ngumu ya maisha ndiyo inayopelekea wao kushindwa kulipa kwa wakati.
Kwa upande wake  Afisa Mawasiliano wa Mamlaka ya Maji safi na usafi  wa mazingira DUWASA Bi Angela  Anton amesema wamekuwa wakiwaonea huruma wananchi kutokana na hali ngumu ya maisha hivyo kuwavumilia katika ulipaji wa bili ya maji lakini kwa sasa wameanzisha mkakati wa kuwakatia wale wote waliolimbikiza bili kwa zaidi ya mwezi mmoja.
Malalamiko haya ya wananchi yanafuatia baada ya mamalaka ya maji safi DUWASA kuanzisha opareshen ya kuwakatia maji au kuwang,olea mabomba wateja wote wenye malimbikizo ya madeni.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive