Tanzania Anthem

Friday, 18 July 2014

NCHIMBI; MKOA WA DODOMA UMESHAMBULIWA NA MBWA VICHAA!!


Mkoa wa Dodoma na wilaya zake unakabiliwa na tatizo  la  kuzuka kwa mbwa wenye ugonjwa wa kichaa wanaowadhuru wananchi na kuwasababishia  madhara  makubwa.

 

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi  alipokuwa akizungumza na Dodoma FM  katika Viwanja vya Nane nane ambapo amesema mpaka sasa takribani watu kumi huripoti  hospitali  kwa  siku  kutokana na kuumwa na mbwa  hao.


Hata hivyo  Dr.Nchimbi amewataka viongozi wa Halmashauri  zote  kuchukua  hatua za  haraka kuwatangazia wananchi wote wa mkoa wa Dodoma  juu ya  kuzuka kwa  wimbi  la  ugonjwa wa Mbwa Kichaa ili waweze kujikinga nao .


Pia ametoa agizo kwa  wamiliki wa  mbwa hao  kuwafungia mbwa wao na kuwapa   chanjo mara kwa mara ili  kupunguza madhara yatokanayo na  ugopnjwa wa mbwa kichaa.


Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive