Tanzania Anthem

Monday, 28 July 2014

RUSHWA YAMALIZA MAZINGIRA KIJIJI CHA MAKULU.


Wakazi wa kijiji cha Hombolo Makulu Mkoani  Dodoma wameilalamikia Serikali ya kijiji kwa kushindwa kudhibiti  tatizo la  uharibifu wa mazingira  katika vyanzo vya maji .

Wakizungumza na kituo hiki wakazi hao  wamesema  tatizo hilo la uharibifu wa mazingira limekuwa likifanywa na watu wanaofahamika katika serikali za mitaa lakini uongozi umeshindwa kulitatua kutokana na kuendekeza rushwa baina yao na waharibifu hao.

Aidha wakazi hao wamesema kutokana na kukabiliwa na tatizo la uharibifu wa mazingira katika vyanzo vya maji  kijijini hapo kunapelekea   mvua kushindwa kunyesha kwa wakati .

Kwa upande wake Afisa Mifugo Mstaafu kijijini hapo Bw. Josephu Moleri amesema hali ya mazingira ni mbaya  kutokana na  viongozi wa eneo hilo kuruhusu baadhi ya watu kufyeka miti kando kando mwa vyanzo vya maji .

Akitoa ufafanuzi juu ya tukio hilo Diwani wa kata ya Hombolo Bw Musa Kawea amesema tatizo la uharibifu wa mazingira ni tatizo la Kitaifa hivyo serikali inapaswa kuongeza maafisa misitu ili kupunguza tatizo hilo la uharibifu katika eneo hilo kwani linakabiliwa na uhaba wa Maafisa Misitu.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive