Uchache wa Shule za Msingi katika Kijiji cha Mpunguzi Mkoani Dodoma umepelekea watoto
wengi kujiingiza katika Ajira.
Haya yamethibitishwa na Diwani wa
kata ya Mpunguzi Bw,.John Matonya alipokuwa akizungumza na kituo hiki kupitia
makala ya amua ambapo amesema kuwa uchache wa shule unapelekea idadi kubwa ya
watoto kutoweza kuandikishwa darasa la kwanza hivyo kuwalazimu kubaki nyumbani
na kujiajiri.
Aidha Bwana Matonya amesema
Halmashauri ina mpango wa kuongeza idadi ya
shule katika Kata hiyo hususani katika Kitongoji cha Mlangwa eneo ambalo lina idadi kubwa ya watoto ambao
hawasomi.
Kwa upande wa wakazi wa Kijiji
hicho wanasema kuwa watoto wengi wanajiingiza katika ajira kutokana na
kutopatiwa mahitaji muhimu na wazazi au
walezi wao.
Hata hivyo watoto
wanaojishughulisha na biashara katika Kijiji hicho wamesema kuwa hali ngumu ya
maisha ya nyumbani inayopelekea
kutokupatiwa Elimu ndiyo inayosababisha wao kujiingiza katika ajira
wakiwa na umri mdogo.
Na Pasko Mwinje Chanzo
DodomaFM
Wamiliki wa vyombo vya usafiri Manispaa ya Dodoma wametakiwa kuhakisha
wanatoa tiketi kwa abiria wanaotumia vyombo hivyo.
Rai hiyo imetolewa na Afisa
Mfawidhi wa Mamlaka ya Usafirishaji Majini na Nchi kavu SUMATRA kanda ya Kati
Dodoma Bw. Bahati Musiba alipokuwa akizungumza na kituo hiki ambapo
amemtaka kila mmiliki wa chombo cha
usafiri ahakikishe anatoa tiketi kwa abiria.
Aidha Bw.Musiba amesema watakao kiuka utaratibu wa kutotoa tiketi kwa abiria mamlaka hiyo
itawachukulia hatua kali za kisheria.
Kwa upande wa Abiria pamoja na
Wamiliki wa vyombo vya usafiri wamesema
suala la tiketi ni muhimu kwani linatoa
utambulisho baina ya abiria na chombo husika.
Na Nazael Mkude Chanzo
DodomFM
Serikali imetakiwa kupunguza matumizi yake ya kawaida kwenye bajeti ya
mwaka wa fedha 2014/15 ili fedha hizo
zipelekwe kwenye miradi ya maendeleo.
Hayo yamesemwa na Mbunge wa Kigoma
Mjini Bwana Peter Serukamba alipokuwa akichangia hotuba ya bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15
iliyowasilishwa bungeni hivi karibuni na Wizara ya fedha na uchumi.
Aidha Bwana Serukamba ameitka
serikali kuchukua maamuzi magumu kuhusiana na suala zima la reli ya kati ili
lipatiwe ufumbuzi wa haraka.
Kwa upande wake Mbunge wa viti
maalumu Bi Leticia Nyerere akichangia hotuba ya bajeti amesema iwapo rasilimali
zilizopo nchini zikitumiwa vizuri itasaidia kupiga hatua kubwa ya maendeleo na kuinua uchumi wa nchi.
Na Lucas Godwin
Chanzo Bunge
KITAIFA
Mahakama
imefanya mabadiliko katika kanuni za uendeshaji wa mashauri ya watoto, kwa kuandaa
kanuni mpya ili kuharakisha usikilizwaji
na uamuzi wa kesi zinazowahusu.
Jaji Mkuu, Mohamed
Chande Othman amesema hayo wakati wa ufunguzi wa warsha ya uendeshaji wa
mashauri yenye masilahi kwa umma kwa majaji wa Mahakama Kuu, iliyofanyika
jijini Dar es Salaam.
Amesema hatua hiyo
imetokana na utafiti uliofanyika katika nchi tatu za Afrika Mashariki kuhusu
uendeshaji wa mashauri yenye masilahi kwa umma ambao umeonyesha kuwa Tanzania
imepiga hatua kubwa.
Jaji Othman amesema mbali na kesi hizo zenye masilahi kwa
umma, kesi nyingine ambazo Mahakama inazipa kipaumbele katika kuhakikisha kuwa
zinashughulikiwa haraka ni kesi za jinsia na watoto.
Na Zania Miraji
Chanzo Mwananchi
KIMATAIFA
Shambulizi
lingine limetokea katika eneo la Mpeketoni karibu na Lamu pwani ya Kenya na kusababisha vifo vya watu
10.
Jeshi
la Polisi limesema washambuliaji wa kundi la Al Shabaab wamekiri kufanya
shambaulizi hilo ambapo walivamia kijiji
kimoja usiku wa kuamkia leo.
Kundi
la Al Shabaab limekiri kuhusika na shambulizi hilo ambapo wameliambia shirika
la habari la Reuters kuwa operesheni yao ya mashambulizi itaendelea nchini
Kenya.
Shambulizi
hili limetokea siku moja baada ya Al Shabaab kukiri kufanya mashambulizi
yaliyowaua watu 50 Jumatatu.
Na
Zania Miraji
Chanzo BBC
Kiongozi wa mashitaka ya umma wa Misri ameamuru
kuachiliwa kwa mwanahabari wa Al-jazeera Abdullah Elshamy kwa misingi ya
kiafya.
Bwana Elshamy ambaye anaripotiwa kudhoofika kiafya alikuwa miongoni mwa
watu 13 ambao mwendesha mashtaka mkuu aliamua kuwaachilia kwa misingi ya kiafya
siku ya Jumatatu ambapo 12 waliosalia ni waliokuwa wakiunga mkono kundi la
Muslim Brother hood.
Bwana Elshamy amekuwa akigoma kula kwa takriban miezi mitano kulalamikia
kukamatwa kwake bila kufunguliwa mashitaka.
Alikamatwa mnamo mwezi Agosti mwaka uliopita wakati polisi wakitawanya
maandamano yaliyokuwa yakifanywa na waandamanaji waliokuwa wakimuunga mkono
rais Mohammed Morsi aliyeondolewa mamlakani.
Stanley msigwa
Chanzo BBC
Marekani imetangaza kuwa inatuma
wanajeshi 275 nchini Iraq kusaidia kulinda maafisa na Ubalozi wake mjini
Bagdad.
Tangazo hilo limetolewa wakati maafisa wa Marekani na Iran wakifanya
mazungumzo kuhusu hali nchini Iraq katika kongamano linalojadili maswala ya nyuklia
mjini Viena.
Rais Obama ameandika barua kwa baraza la Congress kueleza mipango ya kutuma
wanajeshi hao 275 mjini Baghdad ambapo amesema jukumu la kikosi hicho ni
kulinda raia wa Marekani wanaoishi nchini Iraq na mali zao.
Wanajeshi hao wataendelea kukaa nchini humo hadi hali ya usalama
itakapoimarika.
Na Zania Miraji
Chanzo BBC
0 comments:
Post a Comment