Tanzania Anthem

Thursday, 19 June 2014

HABARI ZA LEO NA MATUKIO YA DODOMA FM HAYA HAPA JUNE 19


 

DODOMA

Wakazi wa Kata ya Hombolo  Manispaa ya Dodoma wamelalamika tatizo la uhaba wa maji safi  linalo wakabili  kijijini hapo.

Wakizungumza na Dodoma fm wakazi wa kata ya Hombolo wamesema upatikanaji wa Maji safi umekua mgumu kutokana na watu waliochimba visima na mabomba kuuza maji hayo.

Nae Mwenyekiti  wa serikali ya Kijiji  cha Hombolo Bw.Yared Mtagwa ame kiri kuwepo kwa tatizo la maji kijijini hapo ambapo amesema serikali ya kijiji ipo kwenye mpango wa kutatua  tatizo hilo.

Akizungumzia suala hilo Diwani wa  kata ya Hombolo Bw.Mussa Kawea  amesema  tayari jitihada  zinafanyika na tayari wamekwisha ongea na  Wamisionari ili wameweza kuwasaidia kufufua visima.
Na stanley Msigwa                                                    dodoma fm
 
Serikali imeshauriwa kujipanga kwa kuboresha miundo mbinu ikiwemo barabara pamoja na reli ili kupunguza mfumuko wa bei ya mazao nchini.

Hayo yamesemwa na  mbunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania Bwana Gozbert Blandes alipokuwa akichangia hotuba ya bajeti ya serikali bungeni mji  Dodoma ambapo amesema mfumuko wa bei huchangiwa sana na bei ya vyakula.
Aidha Bwana Blandes ameishauri serikali kuhusiana na fedha za tozo ya umeme vijijini ziwek we kwenye mfuko maalumu ili zifanye kazi  ya umeme vijijini kama serikali ilivyokusudia.
Nae mbunge wa viti maalumu Cecilia Pareso amesema suala la manunuzi ya uma hasa pale kunapokuwepo na warsha au semina liangaliwe na lizibitiwe ili kuondoa ubadhilifu wa fedha za umma.

Serikali imewataka wamiliki na waendesha magari ya mizigo kulinda bima  zao kwa matumizi ya watu wengine barabarani.

Hayo yamesemwa na Naibu waziri wa Fedha Mwiguru Nchemba Wakati Akijibu swali la  mbunge wa viti maalum Mary Chatanda lililohoji  juu  ya baadhi ya malori yanayofanya safari zake  kati yaTanzania na nchi jirani  kukwepa  kulipa kodi kwa kulipa Bima bandia.

Aidha  Waziri Nchemba amesema  sheria  ya bima za magari ya mwaka 2002 inakataza gari lolote nchini kutembea bila bima, na  sheria ya bima ya mwaka 2009 inatoa adhabu kali kwa mmliki atakaebainika kujihusisha  na utengenezaji  au usambazaji wa Bima Bandia.

KITAIFA

Teknolojia ya kisasa inayotumika katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere kukabiliana na dawa za kulevya imeonyesha mafanikio katika kuwabaini wanaojishughulisha na usafirishaji wa dawa hizo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe wakati akifungua semina ya Baraza la Viongozi wa Dini la kupambana na dawa za kulevya Tanzania iliyofanyika  jijini Dares salaam.
Aidha Dr.Mwakyembe amesema teknolojia hiyo imesaidia kupunguza aibu ya watu wanaokamatwa na dawa za kulevya katika nchi nyingine duniani kote wakitokea Tanzania .
Dk Mwakyembe amesema wizara yake ipo katika mchakato wa kutafuta kampuni yenye teknolojia ya kisasa zaidi itakayoimarisha ulinzi na kukabiliana na hila zote za wasafirishaji  ambapo ameaomba ushirikiano wa vyombo vya ulinzi na usalama ili kubaini mtandao wa biashara hiyo.
 KIMATAIFA
Kenya imesema haitaondoa majeshi yake nchini Somalia licha ya kuongezeka kwa mashambulizi ya kigaidi kutoka kwa wapiganaji wa Somalia. 

Naibu rais wa Kenya Bw William Ruto akizungumza na waziri mkuu wa Somalia Bw Abdiweli Ahmed amesema  Kenya haiwezi kuacha majukumu yake yanayoendelea nchini Somalia na kwamba itashirikiana na tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia kuhakikisha kuwa utulivu unapatikana nchini  humo. 

Mbali na hayo habari zinasema  kuwa Kenya na Israel zimeahidi kuimarisha ushirikiano kati yao kwenye mapambano dhidi ya ugaidi .
Na Zania Miraji                                                                                                    Chanzo BBC

Iraq imeomba rasmi usaidizi wa Marekani kushambulia kwa ndege wapiganaji wa kiislamu walioteka miji kadhaa nchini humo wiki hii.
Katika taarifa yake kwa taifa, waziri mkuu Nouri AL Maliki ametoa wito kwa raia wa Iraq  kuungana  dhidi ya wanamgambo.
Vikosi vya jeshi vinajitahidi kuwakabili na kuwasukuma nje wanamgambo wa ISIS pamoja na washirika wao wa Ki-sunni kutoka mikoa ya Diyala na Salahuddin baada ya waasi hao kuteka mji wa Mosul wiki iliyopita.
Taarifa kutoka katika ikulu ya White house zinasema kuwa Rais Obama amependekeza kuongezwa juhudi  nchini Iraq za kusaidia majeshi ya serikali hiyo katika kukabiliana na wanamgambo wa ISIS ikiwemo uwezekano wa kuongeza usaidizi wa kiusalama.
Na zania Miraji                                                                                                      Chanzo BBC

Rais wa zamani wa Liberia, ameanzisha harakati za kisheria kupinga amri ya kutumikia kifungo chake cha jela nchini Uingereza. 

Bwana Taylor amekataa kutumikia kifungo hicho Uingereza akisema kuwa ananyimwa haki ya kufurahia maisha yake  huku  Mawakili wake wakisema kuwa kuzuiliwa kwake nchini Uingereza kunakiuka haki za binadamu.

Mawakili hao wamesema badala ya kutumikia kifungo Uingereza, aruhusiwe kutumikia kifungo hicho nchini Rwanda, pamoja na wafungwa wengine waliohukumiwa na mahakama maalum ya umoja wa mataifa kuhusu Sierra Leone.

Charles Tayor anatumikia kifungo cha miaka hamsini jela kwa makosa ya ubakaji na kutumia watoto kama wanajeshi wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sierra Leone.
Na Zania Miraji                                                                                                            Chanzo BBC
Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive