Tanzania Anthem

Friday, 20 June 2014

STORY KUBWA NA MATUKIO KWA LEO JUNE 20 SOMA..


DODOMA
Wabunge wameendelea kuishauri Serikali juu ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa ajili ya kuwekeza katika maendeleo ya Taifa.


Akichangia mjadala wa Bajeti katika kipindi cha majadiliano Bungeni mjini Dodoma Mbunge wa Kuteuliwa Bw.James Mbatia ameishauri  serikali  iangalie namna ya kupunguza matumizi yasiyokuwa  ya lazima.

Aidha Bw.Mbatia amesema kunavyanzo vingi vya mapato ambavyo vinaweza kutumika vizuri katika kuongeza kipato na kuchangia kwa kiwango kikubwa katika bajeti ya nchi.

Sanjari na hayo amewataka viongozi kuwa mfano bora kwa kulipakodi mbalimbali ikiwemo kodi ya majengo.
Na Pasko mwinje                                                                                           Chanzo Bunge

Pamoja na Tanzania kupiga hatua kubwa katika kupunguza Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama Kwenda Mtoto wananchi wametakiwa kutokujibweteka.

Haya yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bi Rehema Madenge katika uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Maambukizi mapya ya VVU kutoka kwa mama kwenda Mtoto ambapo amesema  Tanzania imepiga hatua kubwa katika kupunguza maambukizi hayo.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa Mkoani Dodoma  Dr   Ezekieli Mpuya  amesema kiwango  cha maambukizi mapya   kitaifa  na  katika mkoa wa Dodoma  kipo juu ,ambapo serikali inashirikiana  na nchi nyingine  kuhakikisha inatokomeza  maambukizi mapya.

Akielezea lengo la uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga maambukizi mapya Mkurugenzii uendeshaji wa Shirika la Tunajali  DR Joseph Ng’weshemi  amesema  lengo ni kuhakikisha  mtoto anayezaliwa na mama mwenye maambukizi anazaliwa  akiwa salama.
Na Stanley Msigwa                                                                   Chanzo Dodoma FM

Imeelezwa kuwa  Rushwa na Matumizi makubwa ya serikali pamoja na bajeti tegemezi ni miongoni mwa maaudui  wa bajeti ya serikali hapa nchini.

Hayo yamesemwa na  Mbunge wa jimbo la Mwibala Bw. Kangi Lugola alipokukuwa akichangia mjadala wa bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2014/15 ambapo ametanabaisha kuwa maadui hao wasiposhughulikiwa bajeti nyingi hazitatekelezeka.

Aidha Bwana Lugola amesema pamoja na serikali kuwa na mpango wa miaka mitano  lakini bajeti zimekuwa zikija tofauti na mpango huo hivyo kusababisha bajeti kutokutekelezeka.
Kwa upande wake Mbunge wa viti maalu kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo  (CHADEMA ) Bw.Christowaja Mtinda amehoji  ni kwanini serikali haijachukua chanzo hata kimoja cha mapato kilichopendekezwa na kamati ya Bajeti.
Na Lucas Godwin                                                                                          Chanzo Bunge

KITAIFA

Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC inatarajia kutumia zaidi ya Sh. bilioni 298 kwa ajili ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa teknolojia mpya ya Biometric Voter Registiration .

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva amesema uboreshaji wa daftari hilo awamu ya kwanza unatarajia kufanyika Mwezi Agosti na Septemba mwaka huu nchini kote.

Bw Lubuva amesema uamuzi wa kuanza kutumia mfumo huo umefikiwa kutokana na changamoto zilizojitokeza katika matumizi ya teknolojia ya Optical Mark Recognition ambao ulisababisha kwa kiasi kikubwa daftari hilo kuwa na kasoro.
Na Stanley Msigwa                                                                                  Chanzo Nipashe

KIMATAIFA

Msemaji wa Umoja wa Mataifa  amesema idadi ya raia wanaotafuta hifadhi katika maeneo ya ulinzi ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini sasa imefikia elfu 95.
Akinukuu takwimu kutoka tume ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini Bw Dujarric amesema zaidi ya watu elfu 30 wapo katika mji wa Juba na wengine elfu 38 wapo kwenye kituo cha Bentiu wakati elfu 18 wapo Malakal huku  wengine wakiwa  katika miji mingine. 

Amefafanua kuwa maeneo mengi yaliyoanzishwa kwa ajili ya kuhifadhi watu wa nchi hiyo yamekamilika au yanakaribia kukamilika, na huko Malakal watu elfu 7 tayari wameshahamia katika maeneo mapya. 

Wasiwasi nchini Sudan Kusini unazidi kutanda na kugeuka kuwa mgogoro baada ya serikali ya rais Salva Kiir kuwatimua wanajeshi wanaomtii makamu wa rais wa zamani Riek Machar na kufanya jaribio la mapinduzi.
Na Zania Miraji                                                                                                  Sauti ya China
Shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR, limesema idadi ya watu waliopoteza makao yao na kufanywa wakimbizi kutokana na vita ni zaidi ya  milioni hamsini.
Idadi hii inasemekana kuwa kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa tangu vita vya pili vya dunia ambapo Takriban watu milioni 17 walitoroka nchi zao na zaidi ya milioni thelathini ni wakimbizi wa ndani ya nchi zao.

Vita nchini Syria, ni moja ya sabab ya kuongezeka kwa idadi hiyo ya wakimbizi, lakini pia kuna mizozo mingine katika Jamhuri ya Afrika ya Kati na nchini Sudan Kusini ambayo imechangia idadi kubwa ya wakimbizi.

Shirika la kuwahudumia wakimbizi  limesema kuwa idadi hiyo ni ishara tosha ya athari za kukosa kuzuia mizozo ambapo limetaka mataifa tajiri  kufanya juhudi kuhifadhi wakimbizi hao
 Na Zania Miraji                                                                                             Chanzo BBC
Katibu mkuu wizara ya mambo ya nje wa Uganda, Balozi James Mugume amesema Uganda haitishwi na vikwazo ilivyowekewa na Marekani kama hatua ya kupinga sheria yake kali kuhusu mapenzi ya jinsia moja.

Serikali ya Uganda imesisitiza kuwa vikwazo hivyo havitakuwa na athari kubwa kwa nchi hiyo na pia imekanusha madai ya mashirika ya kijamii kuwa tayari sheria hiyo imechochea ongezeko la dhuluma dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.

Kadhalika msemaji wa serikali Ofwono Opondo amenukuliwa na shirika la habari la AFP akisema kuwa wananchi wa Uganda wanafahamu kuwa hawatategemea tena msaada wa nchi za Magharibi
Vikwazo ambavyo vimetolewa na Marekani dhidi ya Uganda ni pamoja na kufutilia mbali msaada wa kijeshi, kuwapiga mrufuku baadhi ya maafisa wa serikali ya Uganda kusafiri nje na kupiga tanji mali zao.
Na Zania Miraji                                                                                                 Chanzo BBC
Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive