Tanzania Anthem

Monday, 23 June 2014

Mahakama nchini Misri imewahukumu jela miaka saba wandishi watatu wa habari wa shirika la habari la Al Jazeera waliokuwa wamezuiliwa kwa miezi sita nchini humo.



Dodoma
Vikundi shirikishi vya polisi jamii katika manispaa ya  Dodoma vimeelezea changamoto  mbalimbali zinazowakabili a wakati wa kutoa elimu ya ulinzi na usalama.

Akizungumzana kituo hiki mkaguzi msaidizi wa jeshi la polisi Bw George  Andala amesema baadhi ya wazazi hawapo tayari  kutoa michango  kwa ajili ya kuendeleza  mafunzo hayo  .

Kwa upande wa  wanafunzi walioshiriki  katika mafunzo hayo  ya polisi jamii yaliyo fanyika  katika shule ya Sekondari  Hombolo wamesema wamejifunza mambo mengi ikiwemo kujenga ushirikiano pamoja  na kuwa na  umoja .

Nae Diwani wa kata ya hombolo bw musa kawea amewataka wanafunzi kushirikiana na jeshi la polisi ili kuwa mfano kwa wanafunzi wengine .
Na Nazael Mkude                                                       chanzo Dodoma fm
Serikali Kupitia wizara ya nishati na madini imesema kuwa imepeleka zaidi ya wanafunzi mia mbili nje ya nchi kwa ajili ya mafunzo ya Gesi Asilia.
Akijibu Swali la Mbunge wa  lindi Salimu Baruani, Naibu waziri wa  Nishati na Madini Mh.Charles Kitwanga amesema kuwa  mpango huo unawapeleka wanafunzi nje ya nchi kwa ngazi ya stashada,na  Uzamili,ambao  wote watakuwa wanatumikia sekta hiyo hapa nchini
Aidha waziri kitwanga amesema kuwa wizara ya nishati na madini imekua ikitoa kipaumbele kwa kuwafadhili  wanafunzi  wa maeneo yenye nishati asilia kama mtwara na lindi kupata mafunzo juu ya rasilimali hizo.
Kuhusu tatizo la wanafunzi wengi kutokidhi viwango vya kimataifa mara baada ya kihitimu masomo yao waziri kitwanga amesema kuwa mpaka sasa wameboresha na wanaendelea kuboresha mitaala ya vyuo vya ufundi stadi ili kukidhi hitaji hilo.
Na Stanley Msigwa                                         chanzo Bunge

Serikali imeombwa kuwekeza fedha nyingi kwenye sekta amabazo zinaweza kuliingizia taifa kipato kikubwa.

Ushauri huo umetolewa bungeni na mbunge wa Kigoma kusini Bwana Moses Machali alipokuwa akichangia mjadala wa bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2014/15 unaoendelea mkoani hapa.
Aidha Bwana Machali ameongeza kuwa kwa kuendeleza utaratibu wa kupeleka fedha nyingi kwenye sekta za kihuduma nchi haiwezi kuimarika kiuchumi.
Kwa upande wake bwana Festus Limbu amesema serikali haiwezi kutekeleza miradi mikubwa kwa kutegemea mapato yasiyo kuwa ya serikali na mikopo peke yake ili ipate maendeleo.
KITAIFA
Wakulima wameaswa kuondokana na kilimo cha mazoea, badala yake watumie kanuni bora za kilimo ili  waweze kuongeza kiwango cha uzalishaji na kipato katika familia zao.
Akizungumza  katika maadhimisho ya  Siku ya Wakulima ya uboreshaji wa mimea  jamii ya mikunde yaliyofanyika Kata ya Singe wilayani Babati Mtafiti Mkuu wa Kituo cha Utafiti Seliani Arusha (Sari), Steven Lyimo  amesema ni vema  wakulima wakaachana na kilimo cha mazoea  ili waongeze uzalishaji.

Aidha amesema kutokana na mabadiliko ya tabianchi, wakulima wanalazimika kutumia mbegu za muda mfupi na kati ili waweze kupata wigo mpana wa uchaguzi wa mbegu anapotaka kwenda shambani.

Sanjali na hayo aliwambia wakulima ni vema kupanda aina za mbegu kulingana na kiasi cha mvua mfano   mwaka ambao hakuna mvua unapanda mbegu ya muda mfupi na  mwaka ambao kuna mvua kiasi unapanda mbegu ya muda wa kati na mwaka ambao kuna mvua ya kutosha unapanda ya muda ya muda mrefu.
Na mariamu kasawa                                                                    chanzo Mwananchi

KIMATAIFA
Wachunguzi kutoka jumuiya ya mataifa ya eneo la maziwa makuu wamechapisha ripoti kuhusu mapigano ya hivi karibuni yaliyotokea katika eneo la mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda.
Ripoti hiyo inasema kuwa mapigano hayo yalitokana  na  mzozo wa ardhi kati ya mataifa hayo mawili katika maeneo ya milima miwili.
Wanachama wa tume hiyo walitembelea pande zote mbili za mpaka na kuthibitisha kuwa Rwanda ilikuwa ya kwanza kulalamika kufuatia habari za wanajeshi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuvuka na kuingia nchini Rwanda kwa lengo la kutaka kuiba ngombe.
Ripoti hiyo inasema kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa upande wake inasema kuwa Rwanda mara kwa mara haiheshimu mpaka ulio kati ya mataifa hayo mawili na wanajeshi wake huvuka mara kwa mara na kuingia katika taifa hilo.
Hata hivyo ripoti hiyo inasema kuwa mapigano ya hivi majuzi yanatokana na kutokuwepo mpaka kamili kati ya mataifa hayo mawili.
Na mariamu kasawa                                                                     chanzo BBC
 
 Watu  ishirini wameuawa katika shambulio  lililotokea  katika  kijiji  kimoja kilichopo kaskazini Mashariki mwa Kenya.

Mwandishi wa BBC anasema watu wenye silaha walivamia kijiji cha Gunana katika County ya Wajir mapema siku ya jumapili ambapo mapigano hayo yalizuka kutoka na mgogoro wa mpaka  baina ya koo mbili za Degodia na Gare.

Pamoja na kwamba kuliwahi kutokea mapigano mengine hapo awali lakini hayajawahi kusababisha vifo vya watu wengi kwa mara moja kama ilivyotokea siku ya jumapili.
Mauaji haya yanakuja wiki moja baada ya watu wapatao 60 kuuwawa katika mashambulizi mawili yaliyotokea eneo la Mpeketoni katika pwani ya Kenya lililodaiwa kufanywa na wapiganaji wa Al Shabaab
Na mariamu kasawa                                                                     chanzo BBC

Mahakama nchini Misri imewahukumu jela miaka saba wandishi watatu wa habari wa shirika la habari la Al Jazeera waliokuwa wamezuiliwa kwa miezi sita nchini humo.

Waandishi hao walipatikana na hatia ya kueneza habari za kupotosha na kushirikiana na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Muslim Brotherhood.
Mmoja wa wandishi hao ni Peter Greste, raia wa Australia na ambaye pia alikuwa mwandihi wa habari wa BBC .
Na mariamu kasawa                                                                     chanzo BBC

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive