Tanzania Anthem

Wednesday, 25 June 2014

STORY KUBWA LEO DUNIANI NI HIZI HAPA



KIMATAIFA
Na Mariam  Kasawa
Maafisa wa wizara ya ulinzi nchini Ukraine wamesema kuwa waasi wanaotaka kujitenga ambao wanaiunga mkono Urusi wamelipua ndege iliyokuwa imewabeba wanajeshi wa serikali na kuwauwa watu tisa.


Shambulio hilo lilifanywa karibu na mji wa Sloviansk unaodhibitiwa na waasi mashariki mwa taifa hilo ambapo kwa mujibu wa maafisa wa Ukrain wamesema helkopta hiyo ilipigwa risasi nje ya makao makuu ya Sloviansk .

Kutunguliwa  kwa helikopta hiyo kumetokea muda mfupi baada ya Serikali na upande wa kundi linalotaka kujitenga kutoka kwa Ukraine kutangaza usitishaji wa mapigano. 

Mnamo Jumanne Rais wa Urusi, Vladimir Putin, alitoa wito kwa Wabunge kubadilisha upigaji kura walioufanya mwezi  Machi ambao  uliomruhusu yeye kuwa na mamlaka  ya kuingilia kijeshi maswala ya Ukraine.

Na Mariam  Kasawa
Maelfu ya wafanyakazi wa migodi ya dhahabu nyeupe nchini Afrika kusini wamerudi kazini kufuatia makubaliano ya malipo yao ya miaka mitatu ya kumaliza mgomo ambao umedumu kwa muda wa miezi mitano.

Baada ya kutokuwa kazini kwa muda mrefu wafanyikazi hao watapewa mafunzo na kufanyiwa ukagauzi wa kiafya nahuenda ikachukua miezi kadha kabla ya shughhuli kwenye migodi kurejelea hali ya kawaida.

Mgomo huo unakisiwa kugharimu makampuni hasara ya dola bilioni mbili na kusababasha kudorora kwa uchumi wa afrika kusini.

Wafanyakazi hao hawakupata mshahara waliotarajia wa Rand za Afrika Kusini 12,500 (zaidi ya Dola 1,000) lakini walikubali mkataba wa miaka mitatu ambapo wataendelea kuongezwa mshahara, penisheni, malipo ya nyumba na bima ya Afya.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive