Tanzania Anthem

Wednesday, 25 June 2014

HABARI KUU KITAIFA LEO HIZI HAPA


KITAIFA
Na lucas godwini
Serikali kupitia wizara ya Viwanda imesema hairuhusu kutumia kuni na magogo kwa ajili ya uzalishaji viwandani hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara Bi  Janneth Mbene alipokuwa akijibu swali la mbunge wa viti maalumu Bi Magdalena Sakaya lililohoji ni viwanda vingapi vinatumia kuni na magogo katika uzalishaji na viwanda vingapi vinavyoruhusiwa kutumia nishati hiyo

Aidha Waziri Mbene ameongeza kuwa serikali imekuwa inachukua hatua kali kwa viwanda vyote vinavyokiuka sheria na kanuni ya ukataji wa miti.
Sanjari na hayo Bi. Mbene ametanabaisha kuwa sheria ya misitu ya mwaka 2002 inazuia uvunaji wa miti usio endelevu hivyo viwanda vinavyokiuka masharti ya serikali vitaadhibiwa kwa mujibu wa sheria.
Na happness chesko
Wakazi wa mtaa wa swaswa Manispaa ya  Dodoma  wametakiwa kufahamu  matumizi ya mabwawa ya maji taka katika kilimo cha umwagiliaji.
Wakizungu na Dodoma fm  wakulima wanaolima mbogamboga katika mabwawa hayo ya maji taka wamesema maji hayo yanawasaidia  katika kilimo cha umwagiliaji  kwani wamekuwa wakilima mbogamboga kwaajili ya biashara.

Nae Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa swaswa  Bw. Chares Nyumba amesema hakuna elimu yoyote waliyopewa wakulima hao juu ya matumizi ya maji hayo  hivyo anawaomba wakulima wawe na subira ili waombe mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira waje kutoa elimu.
Akizungumzia suala hilo  Mkuu wa mawasiliano  wa  Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Bw. Sebastiani Warioba amesema  ni vema wakulima hao wakatambua kuwa maji wanayotakiwa kuyatumia ni ya mabwawa ya mwisho kwani ndiyo yanayo ruhusiwa baada ya kujitibu.

Kilimo cha umwagiliaji kinaweza kikaleta tija katika mkoa wa Dodoma kama kitazingatiwa kwa ufasaha hivyo ni vema serikali ikaboresha miundo mbinu ili wakulima waweze kunufaika na kilimo hiki.

Na Stanle Msigwa
Wazazi na  walezi katika  manispaa ya Dodoma wamelezea changamoto zinazopelekekea  ongezeko la  watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Akizungumza na Dodoma fm mlezi wa kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu  (KISEDETI) bw. Kiweku Mpoto amesema wazazi hawatoi ushrikiano hasa kwa watoto katika malezi hivyo kusababisha tatizo hilo.

Nae  bi. Mwashi  Katema  ambaye ni mlezi amesema watoto wanapata tabu kutokana na hali ngumu ya maisha na sababu mbali mbali  zinazo tokea katika jamii zinapelekea hali hiyo kutokea .
Kwa upande wao watoto wanaoishi katika mazingira magumu wameiomba serikali  iwasaidie watoto waliopo mitaani kurudi nyumbani.

Na Livingstone mwangingo
Wakazi wa manispaa ya Dodoma wamelalamikia upandaji wa nauli kiholela katika mabasi yaendayo mikoani hususani kipindi cha likizo.

 Wakizungumza na  Dodoma fm wakazi hao wamesema kupanda kwa nauli   kunachangiwa na  mamlaka ya usafirishaji majini na Nchi kavu (SUMATRA)  kwani imekuwa haitoi taarifa kwa wananchi.

Nae Bw, Dismon Kiwaye amesema kuwa  mamlaka husika inashindwa kusimamia kupanda kwa nauli kiholela kutokana na baadhi ya wafanyakazi wa mamlaka hiyo kumiliki mabasi .

 Akijibu malalamiko hayo  Kaimu Afisa Mfawidhi  wa  mamlaka ya usafirishaji majini na Nchi kavu Bw. Ezekiel Emmanuel amesema wametoa nauli  elekezi ambazo wamiliki wa mabasi wanatakiwa kuzingatia na si kupandisha nauli kiholela.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive