Tanzania Anthem

Friday, 27 June 2014

MAJI TAKA MKOANI DODOMA YAGEUZWA NA KUTUMIKA NA WAKULIMA....


 
 
Na Stanley Msigwa
Kufuatia kauli ya shirika la  maji safi na maji taka pamoja na usafi wa mazingira mkoa wa Dodoma DUWASA  kuwataka wakulima wa mboga katika bwawa la Swaswa kata ya Ipagala katika manispaa ya Dodoma kusitisha shughuli hiyo kutokana na usalama kiafya, wakulima wa eneo hilo watoa maoni juu ya kauli hiyo.

Wakizungumza na kituo hiki Baadhi yao wamedai kuwa  maji taka hayo ndio chanzo Kinachowapelekea wao kuendesha maisha ya kila siku na kudai kuwa kama serikali haita watafutia bwawa jingine hawapo tayari kuacha kilimo hicho.

Nae  mwenyekiti wa mtaa huo bwana Charlse Nyoma amesema kuwa  mtaa huo wenye jumla ya Wakazi zaidi ya elfu Nne na Mia Saba na asilimia kubwa wanategemea kilimo cha umwagiliaji kupitia bwawa hilo.

Aidha bwana nyoma amesema kuwa serikali ina mipango mingi ambayo haitekelezeki na wakati huu wapo kwenye mkakati wa kuzungumza na  DUWASA ili kujua jinsi gani ya kutatua tatizo hilo.

Kwa upande wake Bwa Sebastiani Afisa habari wa  DUWASA amesema kuwa maji hayo si salama kwa matumizi kwani maji hayo yanatokana na matumizi ya watu majumbani na Kutoa tamko la kuwa hayaruhusiwi katika kilimo hicho.  

 
Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive