Tanzania Anthem

Saturday, 5 December 2015

MKURUGENZI MPANDA NA WENZAKE WAFUKUZWA KAZI KWA UPOTEVU WA MAMILIONI.

MKURUGENZI Wa Masnipaa ya Mpanda Bw.Suleiman Lukanga na Watendaji Wengi wa halmshauri hiyo wamesimamishwa Kazi Kutokana na tuhuma za Upotevu wa Shilingi Milioni 92.75.

Uamuzi huo Umechukuliwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahim Msengi  Kutokana na Uchunguzi wa tume tatu zilizoundwa Kuchunguza Upotevu wa Fedha hizo Kati ya Shilingi Milioni 200  Zilizotolewa na Tamisemi Kwa lengo la Kununulia gari la Kubebea taka Katika Manispaa ya Mpanda.

Watendaji wengine Waliosimamishwa Kazi ni Kaimu Mkurugenzi Bw.Vicent Kayombo ambae Pia ni Afisa Elimu Msingi Katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, Afisa Manunuzi Bw,Kakulima Afisa Mipango, Bw Ferdinad Filimbi Mweka hazina, Bw Bosco Kapinga, Mhasibu Kibi Hamis Msaka na Wajumbe wa Bodi ya  Zabuni.

MSIKILIZE KAMANDA WA POLISI KATAVI AKITHIBISHA KUKAMATWA KWA MMOJA WAO KWA MAHOJIANO ZAIDI
Katika Uchunguzi Uliofanywa na Kamati zilizoundwa chini ya Mkuu wa Mkoa, Kamanda wa Polisi Mkoa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru wamebaini Kuwa Kampuni ya Bluecyon iliyoko Mbezi Jijini Dar es Salaam iliyopewa tenda ya Kununua gari hilo haifanyi Biashara ya Magari badala yake ni Kampuini ya Uchapishaji yaani (Printing)

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive