Tanzania Anthem

Tuesday, 4 August 2015

SIMANZI:KIGOGO KAMTELEKEZA MKE NA WATOTO 3 KISA DARASA LA SABA.PART 2


Na-MwandishiWetu,Singida.

MDAI katika Kesi ya madai ya talaka Magreth Mwangu  dhidi yaMkurugenzi wa Shule ya St. Mathew, Thadei Mtembei amehoji uhalali wamahakama kufikia kukagua mali zake siku ya Jumamosi  bila kupitiamahakama yoyote hapa Singida.Kesi hiyo ambayo inasikilizwa mahakama ya Mwanzo Kizuiani MbagalaJijini Dar es Salaam, juzi (Jumamosi) ililazimika kuhamia mkoaniSingida baada ya mdaiwa (Thadei Mtembei) kuitaka mahakama kuhamiamkoani Singida kwa gharama zake ili kuhakiki nyumba ambazo alidaialimjengea Mwangu.Mtembei katika hoja yake ya kuitaka mahakama kuhamia Singida alisemayuko tayari kulipa gharama zote ikiwemo nauli na posho.Hakimu anayesikiliza kesi hiyo Rajab Tamaambele, na wakili wa Mtembeiambaye ni mtoto wa mke mkubwa wa Mtembei (Peter Mtembei), karani nakesi na mtumishi wa mahakama ni miongoni mwa watu waliofika kwa ajiliya ukaguzi na uhakiki wa nyumba hizo.Hata hivyo hakukuwepo na wazee wa baraza jmbo ambalo mwangu pia alililalamikia.Mwangu alidai kuwa licha ya kuwa hafahamu sheria kutokana na kutokuwana elimu hata ya Sekondari lakini kitendo ha mahakama kufika Jumamosikwa ajili ya kufanya uhakiki na ukaguzi haioni kama ni ha haki na piakulikuwa hakuna afisa ustawi wa jamii.Alidai  hakimu kuongozana na wakili wa kesi hiyo na kuwa pamoja mudawote haoni kama atatendewa haki katika shauri hilo.“Mimi nahoji ushirikiano huu kama hautanitendea haki kwani watuwametoka pamoja Dar es Salaam wameongozana kwenye magari binafsinafika eneo la tukio nakuta msafara wa hakimu, wakili wa mdaiwa,mwenyekiti wa kitongoji ukiwa umeshafika mbele ya nyumba ambayowalitaka kuanza kuihakiki” alidai.Alidai hata mwenyekiti wa Mtaa wa Sabasaba, Mahamoud alisema hajapewataarifa yoyote ya maandishi kwani alishtukizwa na kupelekwa kwenyenyumba hiyo ambayo alisema hafahamu kama ni ya Mwangu.Pia alihoji uhalali wa mtoto wa Mtembei ambaye ni wakili kusimamiashauri hilo katika mahakama ya Mwanzo huku mara kadhaa akimtoleamaneno ya kashfa kama ni mfunga vidonda tu hawezi kujenga nyumba.Mwangu alisema alishawahi kuiambia mahakama kuwa nyumba zake zaSingida alizijenga na aliamua kuziuza kwa ajili ya elimu ya watotowake ambao walitelekezwa na baba yao lakini cha kushangaza mahakamakwa amri ya Mtembei ikataka kufika Singida kuhakiki nyumba zake.Hata hivyo mahakama ilikagua nyumba tatu ambapo moja ilikuwaimeshauzwa kwa Sh. Milioni 15 na nyingine iliuzwa ikiwa katika hatuaya msingi.Baada ya kumalizika kwa uhakiki huo hakimu Tamaambele alimtaka Mwangukuhakikisha anawasilisha mahakamani nyaraka zote za nyumba nakuwapeleka watoto mahakamani kabla ya kesi hiyo kutolewa hukumu Agosti25, mwaka huuMwisho


Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive