Tanzania Anthem

Friday, 10 July 2015

MWENGE WASABABISHA BARABARA ZIKARABATIWE


Ukarabati wa barabara ya mto kasimba umeenza kutokana na ujio wa mwenge wa uhuru july 20  mwaka huu.

Mpanda radio fm imzungumza na mwenyekiti wa mtaa wa msasani bw.jonald makoli ambapo amethibitisha  kuwa halmashauri imesha mkabidhi mkandarasi ambaye ameshaanza kuweka kifusi kwa ajili ya kuweka sawa barabara hiyo itakayopitiwa na mwenge wa uhuru mkoani hapa.
Bw.makoli ameongeza kuwa bajeti ya mwenge ndio inayotumika kutengeneza barabara hiyo kutokana na wao kutotengewa bajeti yake.

Sanjari na hayo amewataka wananchi kutokuwa na hofu kufatia kuvunjwa kwa  mabaraza ya madiwani na kusitishwa kwa shughuli za wabunge ambao ndio wawakilishi wa wananchi  kwani shughuli zote za maendeleo zitaenda ipasavyo


Utengenezaji wa barabara ya  inayounganisha mpanda hoteli,msasani,na majengo kupitia mto kasimba umekuja mara baada ya mwenge wa uhuru kutakiwa kukagua na kuzindua ujensi wa maabara katika shule ya sekondari kashaulili ambapo barabara hiyo ndiyo itakayotumika.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive