Tanzania Anthem

Wednesday, 15 July 2015

HABARI PICHA::WAKATI WA SWALA YA JIONI PAMOJA FUTARI AKIWA MKUU WA MKOA NA WENGINE.

MKUU wa Mkoa wa Katavi Dk. Ibrahim Msengi amesisitiza kuwepo kwa amani, upendo na ushirikiano kwani itakuwa ni fursa nzuri kwa watu kufanya shughuli za maendeleo.

Dk. Msengi ametoa kauli hiyo jana katika hafla fupi ya kufuturisha iliyofanyika Ikulu ndogo mjini Mpanda.
Amewataka wakazi wa mkoa wa Katavi kuondoa tofauti za itikadi za kidini na kisiasa na badala yake wadumishe amani na kuepukana na vitendo viovu, kwani Watanzania wote ni wamoja na wanashirikiana katika kila. 

Amewataka wakazi wa mkoa wa Katavi kutoa taarifa kwa vyombo vya dola pindi wanapoona kuna dalili za uvunjifu wa amani ili hatua za haraka zichukuliwe.
Hafla hiyo fupi ya futari, ilihudhuriwa na viongozi wa dini wakiongozwa na askofu wa kanisa la New harvest Afrika mashariki na kati Askofu Laban Ndimubenya, viongozi wa serikali, waumini wa dini mbali mbali na waandishi wa habari. 

TAZAMA PICHA HAPO CHINI>>
Picha zote na Msigwa Stanley









WA PILI KUSHOTO NI MKUU WA MKOA WA KATAVI DR.IBRAHIM MSENGI



SHEIKH MASHAKA AKIONGOZA SWALA








MKUU WA MKOA WA KATAVI (KATIKATI)AKIPATA FUTARI NA VIONGOZI WA DINI YA KIISLAMU-MKOA WA KATAVI

KATIKATI NI ASKOFU LABAN NDIMUBENYA WA NEW HARVEST CHURCH




RPC.MKOA WA KATAVI DHAHIRI KIDAVASHARI AKIFUTURU.



WAWAKILISHI KUTOKA DINI YA KIKIRSTO,WA KWANZA KUSHOTO NI FATHER WA JIMBO KUU LA MPANDA ROMAN CATHOLIKI NACLETUS BAFUMKEKO

MKUU WA MKOA AKISIKILIZA SHUKRANI KUTOKA KWA MWAKILISHI WA SHEIK MKUU KATAVI.(ALIESIMAMA)


MIONGONI MWA WAUMINI WALIO HUDHURIA HAFLA HIYO KATIKA VIUNGA VYA IKULU NDOGO MPANDA MJINI.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive