Tanzania Anthem

Thursday, 2 April 2015

KIKOSI CHA MAANGAMIZI DHIDI YA FC PLUTNUM,SITA WATEMWA.


Basi Lililobeba Mashabiki Wa Yanga Wanaokwenda Kuishangilia Timu Yao Keshokutwa, Tayari Limewasili Nchini Zimbabwe.



Basi Hilo Aina Ya Toyota Costa ‘Mayai’ Limetua Kwenye Mpaka Wa Zimbabwe Leo Asubuhi Na Walitarajia Kukanyaga Ardhi Ya Nchi Hiyo Leo.

Hata Hivyo, Bado Watakuwa Na Safari Ndefu Na Wanatarajiwa Kuwasili Harare Leo Mchana Kabla Ya Kuanza Safari Nyingine Ya Kwenda Bulawayo Ambako Yanga Itapambana Na FC Platinum Katika Mchezo Wa Pili Wa Kombe La Shirikisho.

Mmoja Wa Mashabiki Walio Katika Basi Hilo Amesema Wamekuwa Wakiendelea Vizuri. Msafara Wa Basi Hilo, Pia Yumo Mzee Wa Yanga, Ibrahim Akilimali Ambaye Ameungana Na Vijana Kwenda Kuwapa Nguvu Yanga.


Rais Wa Shirikisho La Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi Amewatakia Kila La Kheri Wawakilishi Pekee Wa Tanzania Kwenye Kombe La Shirikisho Barani Afrika (CC) Young Africans, Katika Mchezo Wa Marudiano Dhidi Ya FC Platinum Ya Zimbabwe Utakochezwa Siku Ya Jumamosi Kwenye Uwanja Mandava Uliopo Gweru Bulawayo.


Malinzi Amesema Young Africans Hawapaswi Kubweteka Na Ushindi Walioupata Awali Wa Mabao 5-1, Kikubwa Wanapaswa Kwenda Kupambana Kusaka Ushindi Ugenini Ili Kuweza Kufuzu Kwa Hatua Inayofuata Ya Timu 16.


Endapo Young Africans Itafanikiwa Kuwatoa FC Platinum Itaingia Katika Hatua Ya 16 Bora Na Itakutana Na Mshindi Kati Ya Timu Za Benifica De Luanda Ya Angola Au Etoile Du Saleh Ya Tunisia.

Kikosi Cha Maangamizi Cha Yanga Dhidi Ya Fc Plutnum Ni Kama

Makipa…Deo Munish Dida’ Ally Mstapha Batez,Mabekiabdul Juma,Oscar Joshua, Pato Ngonyani,Mbutu Twite,Rajab Zahri,Kevin Yondani,Nadri Haroub’’canavaro’’ Viungo Nisalum Telela Nizar Khalfan,Saimon Msuva,Said Juma,Haruna Niyonzima,Mrisho Ngassa,

Na Washambuliaji Ni  Amis Tambwe,Dany Mrwanda,Hussen Javu.

 

Bench La Ufundi Litaongozwa Na Kocha Mkuu Mholanzi Hans Van Der Pruijm ,Kocha Msaidizi Charles Bonface Mkwasa,Kocha Wa Makipa,Juma Ponda Mali,Meneja Hafidh Saleh,Mchua Misuli Jacoub Onyango,Daktari Wa Timu Sufian Juma Na Mtunza Vifaa Mahamoud Omar’’mpogolo’’

Wachezaji Watakao Achwa Katika Mechi Hii Ni Endrew Coutinho,Hassan Dilunga Viungo, Washambuliaji Jerry Tegete,Kpha Sherman Kipa Alphonce Matogo,Charles Edward Beki

Yanga Watafikia Hotel Ya Rainbow Na Jion Watakwenda Kufanya Mazoezi Ili Kuuzoea Uwanja Wa Mandava.


Ili Kusonga Mbele Plutnum Wanatakiwa Kushinda Magoli 4 Kwa 0 Ila Yanga Anatakiwa Kusuruhu Na Namna Yeyote.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive