Tanzania Anthem

Thursday, 11 December 2014

(TAKUKURU);MPOKEA RUSHWA KWENYE UCHAGUZI ANACHO.

Na Martha magawa  ...Dodoma 
Wakati kampeni za uchaguzi  wa serikali za mitaa zinaelekea ukingoni Taasisi Ya Kuzuia Na Kupambana Na Rushwa (TAKUKURU) Imewataka wananchi kutojihusisha na masuala mazima ya kupokea rushwa.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa ( TAKUKURU) Mkoa wa Dodoma  Bi. Emma Kuhanga alipotembelewa na Dodoma fm ofisini  kwa lengo la kutaka kufahamu Taasisi yake imejipangaje kudhibiti vitendo vya kutoa au kupokea rushwa msimu huu wa uchaguzi  kama anavyobainisha.
Aidha Bi .Kuhanga amebainisha adhabu zitakazo tolewa kwa mtuhumiwa ataebainika kupokea au  kutoa rushwa ambapo ni pamoja na kupoteza sifa ya kuwa kiongozi.

Sanjari na hayo amewataka wananchi kupingana na rushwa kwa kutopokea  pamoja na kutoa taarifa mara tu wanapoona tabia ya rushwa inatendeka .
Uchaguzi  wa serikali za mitaa unatarajia kufanyika nchi nzima Desemba 14 mwaka huu hivyo basi TAKUKURU nao hawapo nyuma kuhakikisha zoezi hilo  linafanyika kwa  haki na  usalama.
       
Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive