Tanzania Anthem

Sunday, 17 August 2014

MADEREVA BODABODA;KUOSHA KOFIA NI NGUMU.



 Na Andrew Chaopa   
Madereva bodaboda  Mkoani Dodoma wametakiwa kuwa na utaratibu wa kupiga dawa mara kwa mara kofia  zinazovaliwa na watumiaji wa usafiri huo  ili kupunguza maambukizi ya magonjwa. 


Wito huo umetolewa na Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Rufaa Mkoani Dodoma Dr.Nasoro Mzee  alipokuwa akizungumza na Uhakika Info ambapo amewataka madereva  bodaboda  wote kuzifanyia usafi kofia zao ili kuwakinga watu na maambukizi  ya magonjwa ya ngozi.

Aidha Dr.Mzee  amewashauri abiria  wanaotumia  usafiri huo kuvaa kofia ngumu   ili kupunguza  athari zinazoweza kutokea pindi inapotokea ajali.

Kwa upande wao madereva boda boda  Manispaa ya Dodoma wamepokea kwa shingo upande kauli hiyo  ambapo wamesema ni zoezi gumu kwa upande wao  hivyo  kuitaka serikali kuliangalia suala hili la kuvaa kofia katika maeneo ya karibu

Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive