Tanzania Anthem

Thursday, 28 May 2015

SERIKALI YATAKIWA KUWAANGALIA KWA JICHO LA TATU>>

Na Lutakilwa Lutobeka_Mpanda

Wananchi wanaofanya kazi katika ya kupepeta mchele katika kata ya Mpanda hoteil wilayani Mpanda mkoani KATAVI wameitaka serikali kuwapatia mtaji ili waachane na kazi hiyo kwani ni hatari kwa afya zao.


Akizungumza na waandishi wa habari wa Mpanda redio bi JUSTINA  ANTONY LUSINGE ameesema kuwa serikali imekuwa ikiwafukuza katika shimo hilo hali ya kwamba shimo hilo ndilo linalowawezesha kujipati fedha za kujikimu ikiwa ni pamoja na kuwasomesha watoto wao,kujipatia chakula, mavazi na hata kujenga.


Kwa upande wake bi MWASI ANDREA ameongeza kuwa wanalazimika kuingia katika shughuli hiyo kutokana na kukabiliwa na majukumu mbalimbali hasa ya kielimu licha ya shughuli hiyo kuwa na madhara makubwa kwa binadamu kutokana na vumbi la mapumba hayo.
                                

Hata hivyo bi Mwasi ameishauri serikali iwasaidie kwa hali na mali ili kuyanusuru maisha ya wananchi ho ikiwa ni pamoja na kuwapatia mahindi pamoja na misaada mbalimbali ya kijamii ili waondokane nakazi hiyo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive