Tanzania Anthem

Thursday, 19 February 2015

ZAIDI YA 78 WAREJESHWA TENA>>BOFYA KUSOMA

Licha ya zoezi la kuwarudisha wanafunzi watoro  kwa mkoa wa katavi kufanikiwa kuwarudisha wanafunzi  78 wa Kidato cha kwanza Mpaka cha nne  Katika shule za Sekondari,Ikola,Ilandamilunda,Mpanda ndogo na Kabungu,bado ugumu wa maisha umetajwa kuwa ndio chanzo cha utoro huo.


Wakizungumza na Uhakika Info baadhi ya wakazi wa mpanda hoteli wamesema kuwa uzembe wa wazazi na na ugumu wa maisha  ndio chanzo cha wanafunzi wengi kukatiza masomo.
.
Nao baadhi ya wanafunzi waliokatiza masomo kwa kigezo cha kukosa mahitaji yashule wamesema kukosa kwa mahitaji mhimu ya shule yanapelekea wao kuacha shule na kutafuta vibarua kwa ajili ya kujikimu.

Sanjari na hayo wakazi hao wametoa mapendekezo ya nini kifanyike kwa wazazi wazembe juu ya ufuatiliaji wa maendeleo ya watoto.

Zoezi la  kuwarudisha watoto watoro na walioacha masomo ilianza rasmi tarehe 12 mwezi huu ikiwa ni amri halali kisheria iliyotolewa na mkuu wa wilaya ya mpanda Bw.Pazza Mwamlima


Share:

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive